26 Apr 2016

LEO WATANZANIA WOTE TUNASHEREKEA MIAKA 52 YA MUUNGANO WETU,HII NDIO HISTORIA YA MUUNGANO HUU ULIODUMU KWA MUDA MREFU NA KUDUMISHA AMANI .


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliundwa
mnamo tarehe 26 Aprili, 1964 kwa Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar (inayojumuisha Visiwa
vya Pemba na Unguja). Tanganyika ilikuwa ni
mwendelezo wakoloni la Ujerumani, utawala wa
Waingereza kwa Mamlaka ya Umoja wa Mataifa,
Himaya ya Umoja wa Mataifa chini ya utawala
wa Uingereza na mwisho Taifa huru kuanzia
mwaka 1961 ndani ya nchi za Jumuiya ya
Madola.
Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar ziliingia mkataba wa Muungano mnamo
mwaka 1964 na kuanzishwa Dola ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania. Mkataba huu wa
Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa
Tanganyika, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na
aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid
Amani Karume tarehe 22 Aprili 1964 huko
Zanzibar. Mkataba huo ulithibitishwa na Bunge la
Tanganyika na Baraza la Mapinduzi hapo tarehe
26 Aprili, 1964 na mnamo tarehe 27 Aprili, 1964,
viongozi wa nchi zote mbili walikutana katika
ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es
Salaam na kubadilishana Hati za Muungano.
Sheria za Muungano zilitoa tamko la Jamhuri ya
Muungano katika Ibara ya 4 kwamba:
“Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar zitalazimika, baada ya kuungana na siku
zote baada ya kuungana, kuunganishwa kuwa
Dola ya Jamhuri kwa jina la Jamhuri ya
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar’ (Ibara ya
4 Sheria za Muungano)”
Jina hili la “Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar” lilibadilishwa baadae mnamo tarehe
28 Oktoba, 1964 na kuwa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa kupitia Sheria ya Jamhuri ya
Muungano, Sheria namba 61 ya mwaka 1964.

HILI NDIO DARAJA LA KIGAMBONI,DARAJA REFU AFRIKA MASHARIKI LILILOPEWA JINA LA BABA WA TAIFA.



Mnamo April 19 ya mwezi huu daraja la kigamboni lilizinduliwa rasmi na kuanza kutumika kama ilivyopangwa.Mgeni rasmi katika shughuli izo za uzinduzi wa daraja hili alikuwa mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ndugu John Pombe Magufuli.
Daraja hili la kisasa linalotajwa kuwa ndio daraja refu kuliko yote Afrika mashariki lina urefu wa mita 680 na upana wa mita 27.5.Daraja hili lina barabara sita za magari na barabara moja ya waenda kwa miguu kila upande.
Daraja hili limepewa jina la baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere licha ya watanzania wengi kupendekeza jina la raisi wa sasa mheshimiwa John Pombe Magufuli Lakini mheshimiwa raisi ye mwenyewe akapendekeza jina la mwalimu Nyerere litumike kama jina la daraja hilo.
Asilimia 60 ya ujenzi wa daraja hili imedhaminiwa na mfuko wa hifadhi ya taifa NSSF na asipimia 40 imetolewa na serikali ya jamhuri ya muungano wa  Tanzania.Daraja hili adi kukamilika limegharimu zaidi ya dola za kimarekani 140.





Muonekano wa daraja hill wakari wa usiku.

24 Apr 2016

LIFAHAMU KWA KINA JIWE HILI KUBWA MWANZA,LINAUKUBWA WA HEKARI ZAIDI YA MBILI NA LINAMKUSANYIKO WA MAWE TAKRIBANI ELFU NNE(4000) JUU YAKE.

Source;GSENGO.BLOGSPOT.COM

Njia kuelekea Jiwe Kuu inachangamoto zake ni barabara inayopitika kimtindo.
Taswira kuelekea Jiwe Kuu Kitangiri Mwanza.
Rock City.
Kutoka moja ya vilele vya Jiwe kuu utakuwa na fursa ya kuona maadhari ya Malaika Beach Resort Mwanza.
Team Yangu ya Utalii ikiwa na wadau Bodi ya Utalii Tanzania..
Moja kati ya mawe ya heshima.
Mabango.
Team #iLoveMwanza #JembekaFestival2016 #Jembeka NaVodacom
Bob White katika moja ya angle za Jiwe Kuu ambako kuna mawe ya historia.
Gsengo at the area.
Vijito juu ya jiwe Kuu.
Kileleni Jiwe Kuu.
Juu kabisa Jump Jump zinahusika....
Wow...
safiii......
The view from the top...!!
Hapa ndipo mahala mmoja wa watemi wa Kabila la wasukuma mwenye historia kubwa Mwanamalundi aliketi panaitwa Matako ya Mwanamalundi.
Jiwe Kuu hili ni jiwe moja lenye ukubwa wa kama hekari mbili hivi ambapo juu yake kuna mawe zaidi ya 4000 yaliyojikita sehemu na sehemu kuleta mvuto wa kipekee katika muonekano.
Kutokana na utulivu unaotawala eneo hili na upekee wa mawimbi ya sauti ukimya umesababisha wahubiri na watumishi wa makanisa kulitumia eneo hili kama sehemu ya ibada.
Kona katikati ya mawe upenuni.
Mungu kweli ameumba dunia Jiwe hili ni kama limejiegesha lakini jinsi lilivyojishikiza ni kwaaina ya kipekee kama limejishikiza hivi,, ukadhani linaweza kuanguka lakini kumbe ahata usukume vipi halianguki,
Let us try.....aaaaah wapi.!!!
Blogger Gsengo at the place
Getto juu ya mwamba.
Mnyama huyu anaitwa pimbi akimbii hats akirushiwa jiwe.

HII NDIO 'MANTA RESORT' HOTELI YA KITALII ILIYOJENGWA CHINI YA BAHARI ZANZIBAR KISIWANI PEMBA.

Manta Resort” Hotel hii ya kipekee iliyo visiwani Zanzibar yawa gumzo kwenye Vyombo vya Habari vya Kimataifa...

Ina vyumba chini ya maji na Bei ya kulala kwa siku ni $900 single na a$1,500 double..Hoteli imekua gumzo kwenye vyombo vya habari vya kimataifa na ndio hoteli pekee yenye vyumba vya chini ya maji Barani Africa ambapo mtu akiwa chumbani anaweza ona samaki wakipita nje ya dirisha lake.

Hoteli hii yenye vyumba 16 iitwayo The Manta Resort ikiwa designed by Swedish company Genberg Underwater Hotels kwa mujibu wa CNN.
Yani ukiwa umelala chumbani unaona samaki kabisa kupitia madirisha ambapo gharama yake kulala kwa watu wawili ni dola za Kimarekani 1500 ambayo ni zaidi ya milioni mbili za kitanzania na kwa mtu mmoja ni $900 ambayo inagonga kwenye milioni moja na laki nne hivi.




23 Apr 2016

HICHI NDICHO KITUO CHA REDIO NA TV KITAKACHOIPA HESHIMA LUGHA YA 'KISWAHILII' KWA KUTUMIA LUGHA HII KAMA JINA LA KITUO HICHO.

Afrika Swahili media ni kituo cha Redio na Tv Kinachoipa heshima lugha ya Kiswahili kwa kutumia lugha hio kama jina halisi la kituo hicho yani yani 'SWAILI FM' Na 'SWAHILI TV'.
Kituo hicho kinatarajiwa kufunguliwa ndani ya wiki mbili zijazo nchini hapa ambapo studio za Redio hii zitakua mkoani Morogoro na za TV zitakua Dar Es Salaam.
Kituo hichi kimejizatiti kuajiri vijana wengi wa kitanzania wenye taranta na vipaji mbalimbali kwenye Sanaa hususa Utangazaji.
Frequency za redio hio ni 93.1 Morogoro.

TAZAMA MAKTABA YA SHULE YA MSINGI ALIYOSOMA MWALIMU NYERERE,NI SHULE YA MSINGI MWISENGE

Samani zilizomo ndani ya maktaba hiyo kabla ya kuwekwa vitabu.Maktaba hiyo imejengwa na kuwekwa samani pamoja na vitabu na shirika la HakiElimu ikiwa ni njia mojawapo ya kumuenzi baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Muonekano wa pembeni ndani ya maktaba ya Shule ya Msingi Mwisenge.Mwl Nyerere alisoma shule hii.


Maktaba inavyoonekana kwa nje


Nukuu ya maneno ya Mwalimu Nyerere kuhusu elimu ikiwa ndani ya maktaba

HILI NDIO KABURI LA WAPENDANAO WAWILI WALIOZIKWA PAMOJA HUKU WAMEKUMBATIANA KATIKA KABURI MOJA WILAYANI BAGAMOYO.

Wapendano hao baada ya kukutwa wamekufa
kandokandao ya bahari ya hindi huku wakiwa
wamekumbatiana,walizikwa kwenye kaburi
moja huku wakiwa wamekumbatiana hivyo hivyo
na hili ndio kaburi lao.
Walikutwa wamekufa kwenye uvukwe wa bahari
ya hindi eneo la kijiji cha Kaole wilaya ya
Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

WAPENDANAO wawili mke na mume
walkutwa wamekufa huku wamegandana
kwenye bichi ya ufukwe wa bahari ya hindi kijiji
cha Kaole,Walaya ya Bamoyo Mkoa wa Pwani
na kurazimika kuzikwa kwenye kaburi moja
huku wamekumbatia.
Akizungumza na Mtandao huu Bw Boniface
Sangija'2 Pac' alidai kwamba historia inaonyesha
kwamba wana ndoa hao wapendanao
waliokuwa wakiishi kijiji cha Kaole walikutwa
wamekufa huku wamegandana kwenye ufukwe
wa bahari ya hindi walikoenda kustarehe.
" Hili ni kaburi la wapendanao ambao histori
iliyopo kwenye ofisi za makumbusho ya magofu
haya ya kaole zinaonyesha kwamba wapendanao
hao waliamua kwenda bichi kuogelea bahari ya
hindi eneo hili la Kaole baada ya kuogelea
walikumbatiana eneo la nchi kavu ikiwa ni ishara
ya muendelezo wa upendo wao wa
ukweli"alisema mfanyakazi huona kuongeze
kusema kwamba,
"Histori hiyo imedai kwamba ghafla wanandoa
hao walifikwa na kifo cha ghafla wote wawili
huku wamekumbatiana, wazee wa kalne hiyo 13
waliamua kuwazika kwenye kaburi moja huku
wakiwa wamekumbatiana hivyo hivyo"alisema
mfanyakazi huyo wa eneo hilo la kitalii la Kaole
ambaye kazi yake ni kutoa maelekezo kwa
watalii wa ndani na wale wa nje ya nchi.
Leo makala hii inafika tamati kwenye
makumbusho ya histori za dini ya kiislama
yalipo kijiji cha Kaole Wilaya ya Bagamoyo Mkoa
wa Pwani,kesho makala hii itawaleta histori na
makumbusho wa dini ya kikristo ambayo pia
yako kwenye mji huo wa Bagamoyo eneo la
Misheni .

8 Apr 2016

HICHI NDICHO KITUO CHA TEMBO YATIMA KINACHOPATIKANA ARUSHA NCHINI TANZANIA.


Tanzania ilianzisha kituo cha kwanza cha tembo yatima mjini Arusha.
Kituo hicho kinaifadhi watoto wa tembo waliopoteza wazazi wao kutokana na vitendo vya ujangili au sababu nyengine.
Hatua ya serikali ya kuanzisha kituo hicho inakuja baada ya utafiti wa serikali kubaini kuwa Tanzania hupoteza takriban tembo 30 kila siku.
Kituo hicho kinatoa uangalizi kwa tembo wadogo wapatao 40, na watahifadhiwa mpaka watakapokuwa wakubwa na hatimae kurudishwa katika mazingira yao halisia.
Katika mahojiano ya hivi karibuni na BBC,Aliyekua  waziri wa Utalii wa Tanzania Lazaro Nyalandu alibaini kwamba katika hifadhi ya taifa ya Ruaha pekee, tembo wapatao 12,000 walitoweka katika kipindi cha mwaka mmoja.
Waziri Nyalandu alikiri kwamba kiwango hicho ni kikubwa mno na kwamba kinatia wasiwasi hivyo kuongeza kwamba uchunguzi umefanyika kubaini chanzo cha tatizo hilo.


Mamlaka maalumu ya Umoja wa Mataifa inayojihusisha na wanyama walio hatarini, imesema kwamba takwimu hizo zinaashiria kwamba Tanzania ni kitovu cha ujangili huku pembe za ndovu zikisafirishwa kupitia bandari ya Dar es
Salaam kwenda nchi jirani.
Tangu mwaka 2009, angalau tani 45 za pembe za ndovu zinaaminika kusafirishwa kwa njia za magendo kutoka Tanzania.

MFAHAMU 'NUNGUNUNGU' MOJA YA WANYAMA ADIMU SANA WANAOPATIKANA TANZANIA NA NCHI ZINGINE CHACHE DUNIANI.

Nungnungu ni wanyama wagugunaji wenye ngozi yenye miiba iliyochongoka wanayotumia kujilinda na maadui. Walienea katika ulimwengu wa sasa na ulimwengu wa zamani. Katika wanyama wagugunaji ni watatu kwa ukubwa, wakitanguliwa na capybara na buku. Nungu wana urefu kati ya sm 20 - 25. Uzito wao wakaribia kg 5.4 - 16. Wana umbo la duara, wakubwa na wataratibu kweli.



Nungunungu ni wanyama ambao huwa na rangi mbalimbali zikiwemo kijivu,nyeusi,kahawia ambayo imepauka kwa sababu ya rangi zake na kumfanya kuwa miongoni mwa vivutio vya utalii

Nungu wa dunia ya leo wanaumbo dogo (japokuwa nungunungu wa Amerika ya Kaskazini wanafikia kama sm 85 kwa maelfu na uzito wa kilogramu 18), 

Ni vigumu sana kuweza kuwaona kwa vile wanaishi kwa mashaka sana,maana mara tu wanapoonekana machoni pa watu hushambuliwa na kuwaua kwa sababu mbalimbali.Wengine huwaua kwa sababu ya kuwatuhumu kuwa wanakula mazao yao mashambani.Lakini wengine huwaua kwa sababu wanadai kuwa miiba yake ni dawa.

Nungunungu hupenda kuishi na kufurahia mazingira yenye mapori na misitu ili kujihadhali na ukatilii anaotendewa.Nivigumu sana kumpata mnyama kama Nungunungu katika sehemu zenye nyasi fupi fupi huwa huishi kwe sehemu zenye nyasi ndefu kwa ajili ya usalama wao.

Nungunungu hula chakula ambacho mara nyingi hulimwa na kuandaliwa na binadamu huko mwituni,ambako ndio sehemu sahihi ya maakazi ya Nungunungu.Kutokana na kuharibiwa makazi yao Nungunungu hulazimika kula mazao yaliyolimwa kama mahindi,ndizi,mihogo,na mazao mengine yanayoliwa na binadamu hiyo upelekea kuwa na uadui mkubwa na binadamu na Nungunungu kuona kuwa mazingira alimo binadamu si maeneo sahihi kwa kuishi ns kuendeleza maisha yake yote.Kwa hiyo uhama na kwenda sehemu jingine.

Nungu hupatikana sana katika maeneo ya kawaida na tropiki ya Asia, Italia, Afrika na Amerika ya Kusini na Kaskazini. Nungu huishi kwenye misitu, jangwani sehemu zenye miamba, vilima na nyikani. Baadhi ya nungu wa Dunia Mpya huishi kwenye miti, lakini nungu wa Dunia wa Kale wanakaa ardhini. Nungu huweza kupatikana hata kwenye miamba kwenye ardhi yenye hata urefu wa mita 3700. Nungunungu ni wanyama wa usiku.

Nungunungu hawazaliani kwa wingi sana kama wanyama wengine wanaoishi mwituni hii ni kwa sababu ni wanyama ambao jamii huwatumia sana kwa ajili ya kitoweo pamoja na shughuli nyingine kama dawa ya asili.

Katika Tanzania inasemekana Nungunungu huwapatikana kwa wingi katika mapori mbalimbali likiwemo pori la Nyamunsi lililoko Wilayani Tarime Mkoa wa Mara.Baadhi ya Wenyeji wa sehemu hiyo wanaamini kuwa ngozi ya Nungunungu ni dawa ya watoto wadogo na hivyo waganga wengi huwawinda na kuwatumia kwa lengo la kutibu watu kutokana na imani tofauti katia jamii.Pia Nungunungu anahusishwa sana na uchawi kwani anaaminika kuwa ukimkuta njiani ni ishara ya kutokea kwa jambo fulani baya au zuri.

Nijukumu la sisi Watanzania kuhifadhi makazi ya wanyamapori kwa kuwa ni suala la sisi sote.Wanyamapori hawa ni urithi wetu,kila mmoja wetu atimize wajibu wake kwa nafasi yake ili kuhakikisha uwo wa rasilimali ya wanyamapori na matumizi yake vinakuwa enendelevu.

HII NDIO 'IRENTE VIEW POINT' ILIYOKO LUSHOTO TANGA,MOJA KIVUTIO KIKUBWA SANA AMBACHO WATANZANIA WENGI BADO HAWAJAKITAMBUA.

Hapa ndipo kileleni na Mwonekano wa Irente 
 Hii ni Miamba mikubwa iliyopo Irente na moja ya kivutio kikubwa katika eneo hili kwa upande kwa Kushoto.
Eneo hili wakazi wa Irente wanaliita Pango ambapo watu wengi wanapenda kupigia picha
Hii ni njia ya kuelekea Pangoni 
Ukiwa Juu ndani ya Pango utaona hivi 
Mmoja wa walinzi akiandika akiwakatia risiti wageni mbalimbali waliotembelea eneo hilo.
Muendesjhaji wa blog ya Maliasili zetu  ,Bwana Fredy  akiwa amefika kujionea eneo hilo.

Watu wengi wamekuwa na utaratibu wa kukalili kuwa wanapoambiwa kwenda kufanya utalii basi mawazo yanahamia katika hifadhi za taifa au Fukwe za Bahari, wakati kuna utalii wa kupanda milima,utalii wa uwindaji utalii wa picha, utalii wa kiutamaduni,Utalii wa Ikolojia,utalii wa fukwe,Michezo ya kwenye maji, utalii wa mali kale,utalii wa mikutano,utalii wa matibabu,utalii wa mashambani na utalii wa jiji.

Irente View Point inapatikana katika kijiji cha Irente kilichopo wilayani lushoto mkoani Tanga, eneo hili liligunduliwa na wazee wa kale ambao walikuwa wakifika hapo kwa ajili ya kuomba na kufanya matambiko na wengine walikuwa wakifika katika eneo hilo kwaajili ya kufanya ibada hasa wakati wa sikukuu za Christmas

Eneo hili lina urefu wa Mita 1500 kutoka usawa wa Bahari , ukiwa juu unaweza kuona maeneo mbalimbali vizuri bila usumbufu wowote, pia watalii wengi wamekuwa wakifika eneo hilo kutokana na hali ya hewa kuwa nzuri, kuona Mandhari nzuri hasa wakati wa asubuhi na jioni.

Jinsi ya kufikia ikiwa unatokea upande wowote, fika hadi Mombo, panda daladala Tsh 3,000 mpaka Lushoto mjini baada ya hapo unaweza panda Boda boda Tsh 3,000 au ukachukua Tax Tsh 10,000 , kiingilio ni Tsh 2,000.