19 Jul 2016

ITAZAME SARAFU YA SHILINGI ELFU HAMSINI(50) YA KITANZANIA.

Pichani ni sarafu  yenye thamani ya shilingi elfu hamsini za kitanzania iliyozinduliwa siku ya mapinduzi mwaka huu.
Sarafu hii imetengenezwa 92% na madini ya fedha.

ZIFAHAMU FURSA KUMI(10) ZA MAFANIKIO TANZANIA.


Miezi michache iliyopita Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji Clouds Media Group, Ruge Mutahaba Alizitaja fursa kumi za mafanikio hapa nchini Tanzania baada ya kufanya utafiti kwa muda mrefu.
Ruge Mutahaba alizitaja fursa izo ambazo kila mtu anaweza akazitumia  kwani zinaanzia na mtaji wa kawaida sana wa laki tano(5).
Fursa Namba 1: Biashara kwenye sekta ya Kilimo (Agri business) . Kilimo ndio msingi wa kila kitu, Watanzania wengi wanalima ili wapate chakula ila si kwa ajili ya biashara. Jambo hili linatoa nafasi kwa watu kuweza kuwekeza kwani kupitia Kilimo tutakuwa na viwanda na watu wengi wataweza kujiajiri.
Fursa namba 2: Biashara ya Chakula (Food Business). Fursa hii naitazama kwenye kuongeza dhamani katika biashara na kuzidiwa kujitangaza, usipike tu kwa kawaida, ila ifanye kwa utofauti ikue na kuongeza kipato.
Fursa Namba 3: Biashara katika sekta ya Mauzo, Manunuzi ya rejareja na Usambazaji kupitia njia ya mtandao (Retail – E commerce). Unaweza kutumia mitandao kuuza bidhaa zako na kununua pia. Sio lazima ukutane na mteja ana kwa ana ila kupitia mtandao unaweza kuanza nguo, viatu na vitu vingine.
Fursa namba 4: Biashara katika tasnia ya Habari na Burudani(Media&Entertaiment . Tukiweza kutengeneza film bora zitasaidia kufikisha tasnia hii mbali. Nigeria wamerekodi filamu moja Marekani, ndani ya mwezi mmoja imeuza kopi laki 5. Na wakati wa sisi kuwekeza zaidi na zaidi ili tufikie huko.
Fursa namba 5: Biashara kwenye sekta ya Huduma za Kijamii. Kwa sasa Tunaona Hospitali na Shule nyingi za binafsi na zinafanya vizuri sana. Hi ni nafasi kwetu kuwekeza.
Fursa Namba 6 : Biashara katika Tasnia ya Mitindo na Urembo (Beuty &Fashion). zamani wote kwa mtazamo wetu mwonekano, mvuto ulitokana na fahari ya mtu mwenyewe alichozaliwa nacho, lakini katika ulimwengu wa sasa mwonekano wa mtu ni ‘featuring’ ya vitu vingi sana kuanzia nywele, kucha, make up, fursa zipo nyingi mf. Sasa hivi unaweza kuambiwa kufanya ‘pedicure & manicure’ ni shs elfu 40 hicho ni kimoja tu”Ruge Mutahaba
Fursa Namba 7: Biashara ya Mashamba, Majengo/Mali isiyohamishika (Real Estate) . Tunaona Shule zinaongezeka na Vyuo pia. Hii inatoa nafasi kwa Watanzania kuwekeza kwa kujenga Hostel ambazo zitatoa huduma kwa Wanafunzi na ni kitu cha kudumu.
Fursa namba 8: Biashara katika sekta ya Usambazaji na Usafirishaji (Transport and Logistics).
Fursa namba 9: Sekta ya huduma za kifedha (Financial services) mfano ununuzi wa hisa. “Uelewa kuhusu masuala ya Hisa umekua sana na hii ni fursa nzuri sana kwa Vijana kama wataanza sasa kuwekeza katika Hisa”.
Fursa namba 10: Intaneti na Teknolojia . Mambo mengi sana kwa sasa yanafanyika kupitia mitandao. Watu wanaweza kufanya biashara kupitia mitandao Hii ni nafasi kwetu sisi kuweza kuwekeza. Hii itatupa nafasi ya kujiajiri na pia kwenda na wakati.

12 Jun 2016

HII NDIO ORODHA YA MAKABILA YOTE YANAYOPATIKANA TANZANIA.


Hii orodha ya makabila ya Tanzania inaweza kuwa na matatizo kwenye majina kadhaa, kwa sababu mbalimbali.
Orodha hii inatokana na orodha ya lugha za Tanzania inayopatikana katika Ethnologue, pamoja na tovuti nyingine.
Inawezekana kwamba baadhi ya majina ya makabila ni majina ya lugha au lahaja tu, badala ya makabila, na labda majina mengine yaliandikwa vibaya.
Juu ya hiyo, hakuna ufafanuzi wa wazi kusema kikundi fulani ni kabila au siyo. Vikundi kadhaa katika orodha hii vina wenyeji mamia tu, lakini vikundi vingine vina mamilioni ya watu; labda kila kikundi kinaitwa "kabila," lakini ni jamii za aina tofauti kabisa. Vikundi katika ukurasa huu vimeorodheshwa kuwa vikundi tofauti kutokana na ushahidi kutoka Ethnologue kutofautisha lugha zao.
Hii ni orodha ya makabila ya watu ambao wamekuwa wanaishi tangu zamani katika eneo ambalo sasa linaitwa Tanzania, pamoja na makabila yaliyogawiwa na mipaka baina ya Tanzania na nchi za jirani.
Orodha hii haizingatii makabila yanayoishi katika Tanzania kama wakimbizi tu, hasa kutokana na vita katika nchi za jirani. Vilevile ukurasa huu hauorodheshi vikundi vya wahamiaji kutoka nchi za kigeni, kama wahamiaji au wazao wao kutoka Uarabuni au Uhindi.

3 Jun 2016

KIFAHAMU KWA KINA KIMONDO KILICHODONDOKA TANZANIA,MKOANI MBEYA WILAYANI MBOZI.

TANGU zamani, jamii nyingi duniani zimekuwa zikivichukulia vimondo kama vitu vitakatifu, jamii hizo ni pamoja na Wanyiha wa Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya. Katika jamii zingine duniani imani hizo zimepewa taswira chanya wakati hapa nchini zinapewa taswira hasi.
Wanyiha waliamini katika utakaso kupitia kimondo hicho, imani ikajengeka ya kuosha nyota, lakini baadhi ya watu wakaihusisha zaidi na ushirikina au kuielezea kuwa ni imani potofu, lakini kwa wenyeji wanaamini chuma hicho ni Baraka kutoka kwa Mungu, kama zilivyo jamii zingine duniani.
Vyanzo mbali mbali vya taarifa za kimondo hicho zinabainisha kwamba, tangu kugunduliwa kwake, maelfu ya miaka iliyopita, wenyeji, ambao ni jamii ya kabila la Wanyiha, waliamini kuwa chuma hicho ilikuwa ni zawadi toka kwa Mungu, kwamba hiyo ilikuwa ni Baraka kwao, walizopewa na Mwenyezi Mungu.
Mtazamo huo wa wenyeji, unathibitisha jambo moja la msingi, kwamba imani yao kuhusu kimondo hicho inahusiana na Uungu na sio ushirikina au imani potofu kama inavyoenezwa na baadhi ya watu.
Kuosha nyota na utalii
Mtaalamu wa masuala ya utalii, Fanuel Sabini anaiangalia imani hiyo kwa mtazamo chanya, ambapo anasema ikitumika (imani) vizuri, itachangia kwa kiwango kikubwa kuvutia watalii wengi zaidi badala ya kuiangalia katika mtazamo hasi, kama vile kuijumuisha katika kundi la imani potofu.
“Nchi nyingi zimetumia imani hizo kuvutia watalii, mfano kuna nchi watu hutembelea kwenda kunawa maji tu, ni ya kawaida sana lakini watalii wanamiminika kwa ajili hiyo tu,” anasema Sabini, kisha anahoji,
“Kitendo hicho cha kunawa maji kina tofauti gani na kuosha nyota kwa kunawa maji yaliyowekwa kwenye kimondo cha Mbozi!”
Wadau wa masuala ya utalii wanaitazama imani hiyo ya wenyeji kuhusu kuosha nyota kwa mapana zaidi, kwamba ikitumika pamoja na utoaji elimu ya unajimu itakifanya kimondo hicho kuwa chanzo muhimu cha mapato yatayotokana na watalii wa nje na ndani.
Sabini anaielezea hatua ya kwanza na ya haraka inayotakiwa kufanyika kuwa ni kuanzishwa kwa makumbusho na kituo cha utafiti kuhusu masuala ya unajimu (astronomy), na wakati huo huo kuitangaza imani ya kuosha nyota, na kwa kufanya hivyo, eneo hilo litakuwa kitivo muhimu cha elimu ya vimondo na unajimu barani Afrika.
Vimondo na imani za dini kubwa
Imani zenye kuhusisha vimondo na nguvu za Kimungu haipo kwa jamii hiyo ya kabila la Wanyiha pekee, bali zipo katika jamii za mataifa mbali mbali duniani, ambako vilianguka. Nyingi ya imani za kidini za jamii hizo zinaelezwa kujengwa kwenye matukio ya kuanguka kwa vimondo.
Historia ya vimondo, kama inavyochambuliwa kwenye mtandao wa http://www.meteorite.fr/en/basics/history.htm(link is external) inabainisha pia jinsi vitu hivyo toka angani pamoja na matukio yanayoambatana navyo, vinavyobeba imani ya dini nyingine kubwa duniani.
Inabainishwa na watalaamu wa masuala ya vimondo kwamba kutokana na imani walizonazo jamii mbali mbali kuhusu vimondo hivyo, wamevihifadhi na imani zao kupewa mtazamo chanya, jambo ambalo limezisaidia jamii hizo kuingiza mapato makubwa kupitia utalii.
Imani hizo zimekuwepo tangu zama za kale, ambapo vimondo viliaminika kuwa vitu vitakatifu na jamii mbali mbali za wakati huo duniani.
Mazingira ya kuanguka kwake hapa duniani, ambapo huambatana na mwanga mkali, sauti, kama vile nyota idondokayo, vumbi na kishindo, ni matukio yenye kusababisha hofu kwa wale walioshuhudia, wakiamini kusababishwa na nguvu iliyo juu ya uwezo wa mwanadamu.
Vitu hivyo au hayo mawe, vilihifadhiwa na jamii vilipodondokea, kama vitu vitakatifu, na wenyeji wakayafanya maeneo hayo kuwa matakatifu, wakaabudu na kuyatumia katika shughuli zao mbali mbali za imani zao.
Tafiti mbali mbali zilizofanywa, zinathibitisha imani hizo kuwepo kwa karne kadhaa, ni tangu zama za kale. Ni imani zinazojengwa kutokana na mazingira ya uangukaji wa vimondo hivyo, ambapo huambatana na mwanga mkali na kishindo.
Lilikuwa tukio lenye maajabu kwa mwanadamu wa zama za kale, na hata leo hii, kwa mwanadamu wa kawaida yatakuwa maajabu toka kwa Mungu. Hata hivyo, kwa wanasayansi, wao wanatoa maelezo tofauti yenye majibu ya kitafiti zaidi.
Miongoni mwa simulizi za kiimani inayotumiwa na wanasayansi, ni ile inayomhusu Mtume Paul, https://www.newscientist.com/.../mg22630183-700-falling-(link is external), ambapo inaelezwa kwamba takribani miaka 2000 iliyopita alikutana na tukio lililobadili kabisa mwelekeo wa maisha yake ya kiimani, na inaaminika kuwa ni tukio lililobadili pia hata maisha ya kiimani ya wanadamu wa leo.
Uchambuzi wa tukio hilo unaegemea zaidi katika maandiko yaliyomo kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume, Mlango wa tisa, ambapo inaelezwa kuwa mtu aliyefahamika kwa jina la Saul wakati huo, akiwa njiani kuelekea Damascus, nchini Syria aliona mwanga mkali angani, akapofuka macho na kusikia sauti ya Yesu. Baada ya tukio hilo alibadili jina, akaitwa Paul, na akajiunga na Ukristo.
Hatua hiyo ya Mtume Paul kujiunga na Ukristo baada ya tukio la safari yake ile, linaegemea kwenye imani kuhusu ukuu wa Mungu, na aliendelea kumtukuza huku akilitangaza neno lake kwa wanadamu.
Wanasayansi wanalinganisha maelezo yaliyomo kwenye Biblia kuhusu tukio hilo la Mtume Paul na lile la kimondo cha nchini Urusi la mwaka 2013, hivyo kuhitimisha kuwa kilichomtokea ni kuanguka kwa kimondo pia. Pamoja na ulinganisho wa matukio hayo mawili, wanasayansi wanatumia maelezo kuhusu mwanga kutoka mbinguni, kama inavyoelezewa kwenye Kitabu cha Matendo ya Mitume, mlango wa tisa,http://onlinelibrary.wiley.com/doi/10.1111/maps.12428/abstract(link is external), na kutoa maelezo yao ya kisayansi katika tukio hilo la Mtume Paul.
Wanasayansi kwa upande wao wanaliangalia tukio lile kisayansi zaidi. William Hartmann, mmoja wa waanzilishi wa taasisi ya “Planetary Science Institute in Tucson, Arizona,” anatoa maelezo tofauti kuhusu kilichomtokea Mtume Paul katika safari yake hiyo ya Damascus, kwamba hakikuwa kitu kingine zaidi ya kishindo cha kimondo kilichokuwa kikianguka, kikiambatana na mwanga mkali.
Wataalamu hao wa masuala ya unajimu, wanabainisha mwanga aliouona ndio uliomsababishia upofu, wa muda, kwani baadaye alirudiwa na nguvu zake za kuona.
Kimondo cha Mbozi
Taarifa kwenye mtandao wa Wikipedia, https://en.wikipedia.org/wiki/Mbozi_meteorit(link is external), zinabainisha kuwa kimondo cha Mbozi ni miongoni mwa vimondo nane vikubwa duniani na katika kundi hilo kinashika nafasi ya nne.
Kuna taarifa zinazopishana kuhusu vipimo vya Kimondo cha Mbozi, hata hivyo katika mtandao huo wa Wikipedia inaonyeshwa kuwa kimondo hicho kina urefu wa mita tatu na kimo cha mita moja, huku uzito wake ukikadiriwa kuwa tani 16.
Taarifa ya Mkuu wa Kituo, Mhifadhi Filmerick Basange inaoana na ile iliyopo kwenye mtandao huo kuhusu urefu na kimo, lakini zinatofautiana kwenye uzito ambapo Mhifadhi huyo anasema kimondo hicho kina uzito wa tani 12, ikiwa ni pungufu na zile za kwenye mtandao huo kwa tani nne.
Maelezo ya wenyeji, yaliyopo kwenye kituo hicho, yanamtaja mhunzi hariri kuwa mtu wa kwanza kutoa taarifa za uwepo wa kimondo hicho kwa Mtawala wa eneo hilo, wakati huo, Chief Mwamengo. Hata hivyo, hakuna aliye na uhakika wa mwaka kilipoanguka pamoja na na ule wa kutolewa kwa taarifa hiyo ya kwanza kuhusu uwepo wa chuma hicho kama ilivyotolewa na mhunzi huyo.
Mpima ardhi (land surveyor), W.H. Nolt kutoka Johannesburg nchini Afrka Kusini alifika hapo kwenye kimondo Oktoba, mwaka 1930 na kuwa mtu wa kwanza kuutangazia ulimwengu kuhusu uwepo wa kimondo hicho, hapo kwenye mteremko wa Mlima Marengi uliopo katika Kijiji cha Ndolezi, Kata ya Mlangali, Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.
Kimondo cha Mbozi kinawekwa katika kundi la vimondo vya chuma kikiwa na asilimia 90 ya madini hayo. Hata hivyo kinachoshangaza wenyeji na hata wataalamu ni hali ya eneo kilipo kutokuwepo kwa shimo kubwa au kwa lugha nyingine kasoko au crater kwa Kiingereza.
Maelezo ya kisayansi kuhusu utata, meteoritecrater.com, huo yanabainisha kuwepo kwa sababu za kisayansi zaidi katika umbaji wake.
Hupati tabu sana kukifikia kimondo cha Mbozi. Kinafikika kirahisi kwa kutumia usafiri wa gari, pikipiki, bajaji na hata baiskeli.
Kimondo hicho kinafikika kwa urahisi utokapo jijini Mbeya au Mji wa Tunduma, mpakani mwa Tanzania na Zambia. Kwa kutokea jijini Mbeya, ni kilometa 40 kwa njia ya Barabara Kuu iendayo nchini Zambia, hadi kufika njia panda, kisha unafuata barabara ya vumbi upande wa Kusini ambapo ni mwendo wa kilometa tisa hadi kukifikia.
Jambo la msigi na haraka katika kukiedeleza kimondo cha Mbozi, ni kuanzishwa kwa Makumbusho na Kituo cha Utafiti wa Masuala ya Unajimu (astronomy) ili eneo hilo liwe kitivo cha elimu ya vimondo na unajimu barani Afrika na kuitangaza imani hiyo ya wenyeji ya kuosha nyota.
Muonekano mungine wa kimondo hichi cha mbozi.


6 Mei 2016

MFAHAMU 'GETRUDE CLEMENT ' KIJANA WA KITANZANIA MWENYE MIAKA 16 ALIYEIWAKILISHA VYEMA TANZANIA UMOJA WA MATAIFA KWA KUTOA HUTUBA BORA ZAIDI .


GETRUDE Clement (16) ni mtoto wa
Kitanzania kutoka Mtandao wa
Wanahabari Watoto mkoani Mwanza,
ambaye anakuwa mmoja wa watoto
wachache kuhutubia kwa kujiamini kwa
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
lililokutana jijini New York nchini
Marekani hivi karibuni.
Mtoto huyo anayesoma kidato cha tatu
katika shule ya sekondari ya Mnarani
amekuwa gumzo katika sehemu
mbalimbali duniani, kutokana na hotuba
yake aliyotoa kwa kujiamini mbele ya
marais na viongozi wanaoongoza nchi
wanachama wa baraza hilo. Ni katika
mkutano huo uliohudhuriwa na marais
60 na viongozi wengine wa mataifa
zaidi ya 150 uliohusu masuala ya
Mabadiliko ya Tabianchi, ambapo
mataifa zaidi ya 150 yalitia saini
makubaliano ya kukabiliana na
mabadiliko hayo ikiwemo Taifa la
Marekani.
Awali kabla ya kusoma hotuba yake,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban
Ki moon alimkaribisha Getrude kwa
kusema; “ni furaha yangu kumualika
Getrude Clement ambaye pia ni
mwakilishi wa vijana anayeishi
Tanzania ambaye anawakilisha sauti za
vijana.” Baada ya kufika mbele ya
viongozi hao, aliwasalimia na
kuwaeleza kuwa yeye ni mwakilishi wa
vijana na watoto duniani katika
kuzungumzia mabadiliko ya tabia nchi,
ambapo alielezea hatari yake na
kwamba amekuwa akifanya kazi ya
kufikisha ujumbe huo kwa wananchi juu
ya mabadiliko hayo.
Mchango wa wazazi Akizungumza na
Blogu hii baada ya kurejea nchini wiki
hii, Getrude ambaye ni mtoto wa pili
kuzaliwa katika familia ya Clement
Leon na mke wake Riziki Athumani
wakazi wa Pasiansi mkoani Mwanza
yenye watoto watano, anasema
kujiamini kwake kumetokana na wazazi
wake na ndugu zake kuwa karibu naye.
Wazazi na ndugu hao kwa mujibu wa
Getrude, wamekuwa wakimuunga
mkono kwa yale anayofanya bila
kumkatisha tamaa jambo ambalo
limekuwa likitia chachu katika jitihada
zake binafsi kila wakati.
Anasema alipata fursa ya
kuwawakilisha vijana na watoto
kutokana na kuwa mwanahabari mtoto
wa mkoani humo, ambaye amekuwa
akifanya vipindi vya watoto katika
runinga na redio. Getrude anasema
yeye pia ni mwanachama wa Mtandao
wenye programu zinazozungumzia
mabadiliko ya tabia nchi kwa
kutembelea sehemu zilizoathirika na
kuzungumza na viongozi wa maeneo
hayo.
Anasema ili kupata njia nzuri ya
kukabiliana na mabadiliko hayo,
wanachama wa kikundi hicho pamoja
na viongozi wa maeneo husika kwa
pamoja, hufanya vipindi katika redio au
runinga na kupata maoni ya watu. Binti
huyo anasema pia kikundi hicho kwa
kushirikisha maoni yao, wamekuwa
wakiwaeleza namna bora ya
kukabiliana na mabadiliko ya tabia
nchi.
Anasema hotuba hiyo aliyoitoa UN,
aliiandaa mwenyewe katika Baraza la
Watoto mkoani Mwanza, baadaye
ikafanyiwa marekebisho na watu
mbalimbali wakiwemo viongozi wake
wa baraza hilo. Mwanafunzi huyo
anayetoka shule ya Serikali, ambazo
zimekuwa zikituhumiwa kushindwa
kutoa elimu bora, anasema mwalimu
mzuri wa somo la Kiingereza na
ufuatiliaji wake wa masomo hayo,
vimemwezesha kusoma kwa umakini
hotuba ile ingawa si kwamba anajua
sana lugha hiyo bali alikuwa akiisoma
mara kwa mara.
Hotuba hiyo kwa mujibu wa binti huyo,
haikuandaliwa muda mrefu kwani
aliandika mwanzoni mwa Machi mwaka
huu kisha kufanyia mazoezi ya mara
kwa mara wakati alipokuwa na uhakika
wa kwenda kuisoma mbele ya viongozi
hao wakuu.
“Kwa kweli niliambiwa kuwa nitasoma
kwa viongozi wakuu lakini sikujua kama
watu watakuwa wengi kiasi kile kiasi
ambapo mara baada ya kutangazwa
kusoma hotuba nilipata hofu lakini kadri
nilivyokuwa nikiendelea kuisoma, niliona
nawasomea watu wa kawaida,”
anasema kwa kujiamini. Anasema tabia
yake ya kutokuwa na hofu, imetokana
na kujiamini kwani amekuwa akifanya
vipindi mbalimbali vya watoto na
amekuwa na jitihada za kuhakikisha
anafanikiwa kwa kila kilicho mbele
yake.
Akizungumzia mipango yake ya
baadaye, Getrude anayesema anapenda
masomo ya sayansi, anasema
anapenda kuwa Mtangazaji wa
kimataifa kwa kuwa anapenda kazi hiyo
anayofanya kila wakati na tayari
ameshaanza kukabiliana na
changamoto zake akiwa mtoto.
Anamtaja mtangazaji anayemvutia
kuwa ni Salim Kikeke wa Shirika la
Utangazaji la Uingereza (BBC) na
wengine wengi wa nchini huku
akisisitiza kuwa kazi hiyo imemfanya
afanikiwe kushiriki masuala mbalimbali
katika jamii.
Ushauri kwa watoto, wazazi Anawataka
watoto nchini kufuata kila
wanachoelekezwa na walimu au wazazi
wao kwa kuwa na nidhamu huku
wakishiriki katika makundi mbalimbali
ya watoto na vijana. “Makundi haya
licha ya kukuongezea ufahamu, pia
yatakupa fursa mbalimbali za kukutana
na watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kupata fursa za kukuwezesha kujiamini
zaidi,” anasisitiza.
Anasema pia wazazi wanapaswa kuwa
karibu na watoto na kuwaruhusu
kushiriki katika makundi mbalimbali,
kwani wazazi wana nafasi kubwa ya
kuwafanya watoto wawe wa aina fulani
ikiwa ni pamoja na kuwaepusha
kushiriki katika makundi mabaya.
Ushauri kwa Serikali Getrude anaishauri
Serikali ya Tanzania kuanza kuchukua
hatua kwa kushirikiana na wananchi
wake kuwapa elimu ya kutosha kuhusu
mabadiliko ya tabia nchi na hiyo ndiyo
itakuwa zawadi kubwa kwake kama
mwakilishi wa nchi.
“Hii itanifanya nijione yale niliyowataka
viongozi wayafanye, yamefanyiwa kazi
kwa uhakika lakini nahisi haya
yatafanyiwa kazi na nchi zote kutokana
na mwitikio wa viongozi hao niliopata
mara baada ya kusoma,” anasisitiza.
Mtoto huyo aliyerejea wiki hii kwa
wazazi wake mkoani Mwanza alipata
mapokezi makubwa huku akieleza kwa
jinsi vyombo mbalimbali vya habari vya
kitaifa na kimataifa walivyomtafuta na
kumhoji.
Watanzania wametoa pongezi nyingi
kwa Getrude na kusema ni hazina ya
nchi, hadi sasa kwani amesaidia
kuitangaza nchi duniani kutokana na
hotuba hiyo aliyotoa mbele ya Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ki-moon.
Akizungumzia safari yao, Katibu Mkuu
wa Shirika la Mtandao wa Watoto na
Vijana Mwanza, Brightius Titus
anasema walimuandaa vizuri mtoto
huyo kwa kufanya mazoezi katika
ukumbi huo siku moja kabla ya
mkutano.
Anasema mara baada ya kutoa hotuba
hiyo watu kadhaa walimfuata
kumpongeza akiwa njiani kuelekea
hotelini na hata alipofika. Titus
anasema nia ya shirika hilo ni
kuendeleza jitihada za mtoto huyo kwa
kumpa nafasi ya kwenda mbele zaidi
na kuwa mfano kwa watoto na vijana
wa Kitanzania. Anamshukuru Balozi wa
Tanzania nchini Marekani kwa kumuita
nyumbani kwake na kumpongeza
pamoja na ofisi ya Makamu wa Rais
iliyomuita katika ofisi hizo mara tu
baada ya kuwasili nchini.
Baada ya kuwasili serikali ilitoa pongezi kwa kumuarika kushuhudia kikao kimoja cha byngr na pia mmoja ya waziri wa jamhuri ya muungani wa Tanzania ameahidi kumsomesha binti huyu.

1 Mei 2016

MFAHAMU 'MOHAMMED IQBAL' MTU ALIEBUNI NENO 'TANZANIA' MPAKA KUTUMIKA KAMA JINA LA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR.

Huyu bwana aliyebuni jina la Tanzania ni
Muhindi na dini yake ni AHMADIYA MUSLIM. Majina yake
ni MOHAMMED IQBAL DAR.
Mohammed alizaliwa Mkoani Tanga miaka
ya 1944,Baba mzazi wa Mohammed
alikuwa Daktari huko mkoani Morogoro
alikuwa anaitwa Dr. T A DAR alikuwa
Tanganyika kuanzia mwaka 1930.
Mohammed Iqbal Dar alipata elimu yake
ya Msingi Mkoani Morogoro shule ya
Msingi H H D AGAKAN kwa sasa ni Shule
ya Serikali na baada ya Hapo alikuja
baadae kujiunga na Chuo cha Mzumbe
akasoma Kidato cha Kwanza mpaka cha
Sita.
Aliingiaje kwenye shindano la
kupendekeza jina la Muungano kati
Tanganyika na Zanzibar,Mohammed
anasema alikuwa Maktaba akijisoma
gazeti la Tanganyika Standard siku hizi
Daily News akaona Tangazo linasema
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
unafahamika kama Republic of
Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana
refu sana kwa hiyo Wananchi wote
wakaombwa Washiriki kwenye shindano la
Kupendekeza jina moja litakalo zitaja nchi
zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar
Mohammed Iqbal Dar anasema aliamua
kuingia kwenye Shindano na hivi ndivyo
alianza Safari ya Kubuni Jina la
Muungano,Kwanza anasema alichukua
karatasi akaandika Bismillah Raahman
Rahimu hii ni kutokana na Imani yake na
baada ya hapo akaandika jina la
Tanganyika baada ya hapo akaandika
Zanzibar halafu akaandika jina lake Iqbal
halafu akaandika jina la Jumuiya yake ya
Ahmadiya baada ya Hapo akamrudia tena
Mwenyezi Mungu akamwomba amsaidie ili
apate jina zuri kutoka katika majina hayo
aliyokuwa ameyaandika.
Baada ya hapo Mohammed Iqbal Dar
alichukua herufi tatu kutoka Tanganyika
yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar
akachukua Herufi tatu za Mwanzo ZAN
ukiunganisha unapata TANZAN alivyoona
hivyo akachukua I herufi ya kwanza katika
jina lake la Iqbal na akachukua A kutoka
jina la dini yake yaani Ahmadiyya kwa
maana hiyo ukiongeza herufi hizi mbili I na
A kwenye TANZAN unapata jina kamili
TANZANIA akalisoma jina akaliona ni zuri
lakini akajiridhisha pia kwamba akiongeza
herufi hizo za I na A kwenye TANZAN
italeta maana kwakuwa nchi nyingi za
Afrika zinaishia na IA.
mfano
EthiopIA, ZambIA,NigerIA,TunisIA,SomalIA,GambIA,NamibIA,LiberIA,MauritanIA
alivyoona hivyo akaamua apendekeze
kuwa jina TANZANIA ndio litumike
kuwakilisha nnchi hizi mbili yaani
Tanganyika na Zanzibar kwa maana hiyo
jina TANZANIA limezaliwa kutoka majina
manne majina hayo ni
Tanganyika,Zanzibar,Iqbal na Ahmadiyya
Mohammed Iqbal Dar baada ya kupata
jina hilo akalituma jina hilo kwenye kamati
ya kuratibu Shindano
Baada ya Muda mwingi kupita baba yake
na Mohammed Iqbal Dar alipokea Barua
nzito kutoka serikalini ikiwa inasomeka
kama ifuatavyo….
REPRESENTED BY THE
MINISTRY OF
INFORMATION AND TOURISM,TANZANIA
TO
MOHAMED
IQBAL DAR
IN RECOGNATION OF THE
ACHIEVEMENT OF CHOOSING THE NEW
NAME FOR THE
UNITED REPUBLIC
OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR NAMELY
“REPUBLIC
OF TANZANIA”
DURING THE NATIONAL
COMPETITION DAY IN 19 TH NOVEMBER
1964
I A
WAKAL
MINISTER FOR
INFORMATION AND TOURRISM
Barua hiyo pia ilisema..
Utakumbuka kuwa miezi michache iliyopita
ulituandikia kutupa ushauri kuhusu jina
jipya la Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar na wewe pamoja na wananchi
wenzio 16 ulishauri nnchi yetu iitwe
Tanzania.Nafurahi kukuarifu kuwa
mshirikiane ile Zawadi y ash.200
iliyoahidiwa na leo nakuletea check ya
sh.12/50 ikiwa ni hisa yako katika zile
sh.200.Nashukuru sana kwa jitihada ya
kufikiri jina la Jamuhuri yetu
Barua ikasainiwa na Idrisa Abdul Wakil
Waziri wa Habari na utalii kipindi hicho.
Sasa kwa nini Mohamedi Iqbal Dar anadai
yeye kuwa mshindi pekee wakati Barua
ilikuwa inaonyeshakulikuwa na washindi
wengine 15 ambao nao walishinda,Jibu ni
kuwa wakati wa kutolewa kwa Zawadi hizo
hakuna aliyejitokeza zaidi ya Bwana
Mohammed Iqbal Dar na Bwana Yusufal
Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa
sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya
kumpongeza kuwa ameshinda kwa madai
kuwa Barua ameipoteza,hivyo Wizara ya
Habari na Utalii iliamua kumtangaza
bwana Mohammed Iqbal Dar kuwa Mshindi
na kumpatia zawadi yote y
ash.200/:pamoja na Ngao.
Bwana Mohammedi Iqbal Dar anasema
anachosikitika ni kuwa Mchango wake
bado Watanzania hawathamini mchango
wake lakini yeye anaipenda Tanzania na
anajivunia kuwa Mtanzania japo anadhani
dini yake ya Uislamu ndio tatizo hawataki
kutambua mchango wake ila anaamini
kuwa siku moja ukweli utajulikana
Hayo ni maelezo ya Mohammed Iqbal Dar
ambaye kwa sasa anaishi Uingereza kwa
kuwa huko ndiko alipata kazi eneo la
Birmigham b35 6ps UK,Dar –es-Salaam
House,18 TURNHOUSE ROAD,PHONE 44
121-747-9822.

26 Apr 2016

LEO WATANZANIA WOTE TUNASHEREKEA MIAKA 52 YA MUUNGANO WETU,HII NDIO HISTORIA YA MUUNGANO HUU ULIODUMU KWA MUDA MREFU NA KUDUMISHA AMANI .


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliundwa
mnamo tarehe 26 Aprili, 1964 kwa Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar (inayojumuisha Visiwa
vya Pemba na Unguja). Tanganyika ilikuwa ni
mwendelezo wakoloni la Ujerumani, utawala wa
Waingereza kwa Mamlaka ya Umoja wa Mataifa,
Himaya ya Umoja wa Mataifa chini ya utawala
wa Uingereza na mwisho Taifa huru kuanzia
mwaka 1961 ndani ya nchi za Jumuiya ya
Madola.
Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar ziliingia mkataba wa Muungano mnamo
mwaka 1964 na kuanzishwa Dola ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania. Mkataba huu wa
Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa
Tanganyika, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na
aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid
Amani Karume tarehe 22 Aprili 1964 huko
Zanzibar. Mkataba huo ulithibitishwa na Bunge la
Tanganyika na Baraza la Mapinduzi hapo tarehe
26 Aprili, 1964 na mnamo tarehe 27 Aprili, 1964,
viongozi wa nchi zote mbili walikutana katika
ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es
Salaam na kubadilishana Hati za Muungano.
Sheria za Muungano zilitoa tamko la Jamhuri ya
Muungano katika Ibara ya 4 kwamba:
“Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar zitalazimika, baada ya kuungana na siku
zote baada ya kuungana, kuunganishwa kuwa
Dola ya Jamhuri kwa jina la Jamhuri ya
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar’ (Ibara ya
4 Sheria za Muungano)”
Jina hili la “Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar” lilibadilishwa baadae mnamo tarehe
28 Oktoba, 1964 na kuwa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa kupitia Sheria ya Jamhuri ya
Muungano, Sheria namba 61 ya mwaka 1964.