31 Mac 2016

HUYU NDIYE TWIGA MWENYE ULEMAVU WA NGOZI[ALBINO /KISAYANSI ANAITWA 'OMO'] ANAYEPATIKANA TANZANIA ,MKOANI ARUSHA KATIKA MBUGA YA TARANGILE.

Twiga huyu mwenye ulemavu wa ngozi ambae kisayansi anajulikana kwa jina la 'OMO' aligunduliwa na Dk.Derek Lee katika mbuga ya TARANGIRE,Mkoani Arusha  wakati dokta huyo akifanya  uchunguzi na utafiti wa wanyama mbalimbali.
Dk.Lee alimgundua twiga huyu mwenye ulemavu wa ngozi kutokana na utofauti wake na twiga  wenzake ambao wanapatikana katika mbuga hiyo.Twiga huyu alioneakana akiongozana na twiga  wenzake sehemu mbalimbali za mbuga hiyo bila ya twiga wenzake kumshangaa wala kumtenga twiga huyu Albino.
 Mnyama huyu ni mnyama  alietofauti sana na wanyama wenzake katika kipengele cha rangi kwani rangi yake ni ile nyeupe ya kukolea inayofanana kabisa na rangi ya binadamu mwenye ulemavu wa ngozi.
Gazeti moja la kimarekani lilitoa ripoti kwamba twiga wa aina hii yani mwenye ulemavu wa ngozi ni wachache sana hapa duniani na kama twiga huyu atatunzwa vizuri basi atakuja kuwa moja ya kivutio kikubwa sana cha utalii hapa duniani.
Licha ya kutokutengwa na twiga wenzake lakini twiga huyu yuko katika hatihati ya kuhuliwa na wanyama wenzake tofauti na swala kutokana na muonekano wa tofauti na wenzake kitu ambacho kina watisha baadhi ya wanyama wenzake.
DK.Leek alisema twiga huyu anatakiwa kupewa ulinzi wa kutosha ili kumzuia kujeruhiwa vikali au kuhuliwa kabisa na wanyama wenzake.Pia DK.Leek alisema mnyama huyu yuko katika hatihati ya kuuliwa na baadhi ya binadamu kutokana na mwonekano unaoweza kuwafanya baadhi ya binadamu kutamani kujua radha aliyonayo mnyama huyu endapo ataliwa kama chakula.


Pichani ni twiga huyu albino 'OMO' akiwa mbugani TARANGILE ,mkoani Arusha.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni