6 Mei 2016

MFAHAMU 'GETRUDE CLEMENT ' KIJANA WA KITANZANIA MWENYE MIAKA 16 ALIYEIWAKILISHA VYEMA TANZANIA UMOJA WA MATAIFA KWA KUTOA HUTUBA BORA ZAIDI .


GETRUDE Clement (16) ni mtoto wa
Kitanzania kutoka Mtandao wa
Wanahabari Watoto mkoani Mwanza,
ambaye anakuwa mmoja wa watoto
wachache kuhutubia kwa kujiamini kwa
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
lililokutana jijini New York nchini
Marekani hivi karibuni.
Mtoto huyo anayesoma kidato cha tatu
katika shule ya sekondari ya Mnarani
amekuwa gumzo katika sehemu
mbalimbali duniani, kutokana na hotuba
yake aliyotoa kwa kujiamini mbele ya
marais na viongozi wanaoongoza nchi
wanachama wa baraza hilo. Ni katika
mkutano huo uliohudhuriwa na marais
60 na viongozi wengine wa mataifa
zaidi ya 150 uliohusu masuala ya
Mabadiliko ya Tabianchi, ambapo
mataifa zaidi ya 150 yalitia saini
makubaliano ya kukabiliana na
mabadiliko hayo ikiwemo Taifa la
Marekani.
Awali kabla ya kusoma hotuba yake,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban
Ki moon alimkaribisha Getrude kwa
kusema; “ni furaha yangu kumualika
Getrude Clement ambaye pia ni
mwakilishi wa vijana anayeishi
Tanzania ambaye anawakilisha sauti za
vijana.” Baada ya kufika mbele ya
viongozi hao, aliwasalimia na
kuwaeleza kuwa yeye ni mwakilishi wa
vijana na watoto duniani katika
kuzungumzia mabadiliko ya tabia nchi,
ambapo alielezea hatari yake na
kwamba amekuwa akifanya kazi ya
kufikisha ujumbe huo kwa wananchi juu
ya mabadiliko hayo.
Mchango wa wazazi Akizungumza na
Blogu hii baada ya kurejea nchini wiki
hii, Getrude ambaye ni mtoto wa pili
kuzaliwa katika familia ya Clement
Leon na mke wake Riziki Athumani
wakazi wa Pasiansi mkoani Mwanza
yenye watoto watano, anasema
kujiamini kwake kumetokana na wazazi
wake na ndugu zake kuwa karibu naye.
Wazazi na ndugu hao kwa mujibu wa
Getrude, wamekuwa wakimuunga
mkono kwa yale anayofanya bila
kumkatisha tamaa jambo ambalo
limekuwa likitia chachu katika jitihada
zake binafsi kila wakati.
Anasema alipata fursa ya
kuwawakilisha vijana na watoto
kutokana na kuwa mwanahabari mtoto
wa mkoani humo, ambaye amekuwa
akifanya vipindi vya watoto katika
runinga na redio. Getrude anasema
yeye pia ni mwanachama wa Mtandao
wenye programu zinazozungumzia
mabadiliko ya tabia nchi kwa
kutembelea sehemu zilizoathirika na
kuzungumza na viongozi wa maeneo
hayo.
Anasema ili kupata njia nzuri ya
kukabiliana na mabadiliko hayo,
wanachama wa kikundi hicho pamoja
na viongozi wa maeneo husika kwa
pamoja, hufanya vipindi katika redio au
runinga na kupata maoni ya watu. Binti
huyo anasema pia kikundi hicho kwa
kushirikisha maoni yao, wamekuwa
wakiwaeleza namna bora ya
kukabiliana na mabadiliko ya tabia
nchi.
Anasema hotuba hiyo aliyoitoa UN,
aliiandaa mwenyewe katika Baraza la
Watoto mkoani Mwanza, baadaye
ikafanyiwa marekebisho na watu
mbalimbali wakiwemo viongozi wake
wa baraza hilo. Mwanafunzi huyo
anayetoka shule ya Serikali, ambazo
zimekuwa zikituhumiwa kushindwa
kutoa elimu bora, anasema mwalimu
mzuri wa somo la Kiingereza na
ufuatiliaji wake wa masomo hayo,
vimemwezesha kusoma kwa umakini
hotuba ile ingawa si kwamba anajua
sana lugha hiyo bali alikuwa akiisoma
mara kwa mara.
Hotuba hiyo kwa mujibu wa binti huyo,
haikuandaliwa muda mrefu kwani
aliandika mwanzoni mwa Machi mwaka
huu kisha kufanyia mazoezi ya mara
kwa mara wakati alipokuwa na uhakika
wa kwenda kuisoma mbele ya viongozi
hao wakuu.
“Kwa kweli niliambiwa kuwa nitasoma
kwa viongozi wakuu lakini sikujua kama
watu watakuwa wengi kiasi kile kiasi
ambapo mara baada ya kutangazwa
kusoma hotuba nilipata hofu lakini kadri
nilivyokuwa nikiendelea kuisoma, niliona
nawasomea watu wa kawaida,”
anasema kwa kujiamini. Anasema tabia
yake ya kutokuwa na hofu, imetokana
na kujiamini kwani amekuwa akifanya
vipindi mbalimbali vya watoto na
amekuwa na jitihada za kuhakikisha
anafanikiwa kwa kila kilicho mbele
yake.
Akizungumzia mipango yake ya
baadaye, Getrude anayesema anapenda
masomo ya sayansi, anasema
anapenda kuwa Mtangazaji wa
kimataifa kwa kuwa anapenda kazi hiyo
anayofanya kila wakati na tayari
ameshaanza kukabiliana na
changamoto zake akiwa mtoto.
Anamtaja mtangazaji anayemvutia
kuwa ni Salim Kikeke wa Shirika la
Utangazaji la Uingereza (BBC) na
wengine wengi wa nchini huku
akisisitiza kuwa kazi hiyo imemfanya
afanikiwe kushiriki masuala mbalimbali
katika jamii.
Ushauri kwa watoto, wazazi Anawataka
watoto nchini kufuata kila
wanachoelekezwa na walimu au wazazi
wao kwa kuwa na nidhamu huku
wakishiriki katika makundi mbalimbali
ya watoto na vijana. “Makundi haya
licha ya kukuongezea ufahamu, pia
yatakupa fursa mbalimbali za kukutana
na watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kupata fursa za kukuwezesha kujiamini
zaidi,” anasisitiza.
Anasema pia wazazi wanapaswa kuwa
karibu na watoto na kuwaruhusu
kushiriki katika makundi mbalimbali,
kwani wazazi wana nafasi kubwa ya
kuwafanya watoto wawe wa aina fulani
ikiwa ni pamoja na kuwaepusha
kushiriki katika makundi mabaya.
Ushauri kwa Serikali Getrude anaishauri
Serikali ya Tanzania kuanza kuchukua
hatua kwa kushirikiana na wananchi
wake kuwapa elimu ya kutosha kuhusu
mabadiliko ya tabia nchi na hiyo ndiyo
itakuwa zawadi kubwa kwake kama
mwakilishi wa nchi.
“Hii itanifanya nijione yale niliyowataka
viongozi wayafanye, yamefanyiwa kazi
kwa uhakika lakini nahisi haya
yatafanyiwa kazi na nchi zote kutokana
na mwitikio wa viongozi hao niliopata
mara baada ya kusoma,” anasisitiza.
Mtoto huyo aliyerejea wiki hii kwa
wazazi wake mkoani Mwanza alipata
mapokezi makubwa huku akieleza kwa
jinsi vyombo mbalimbali vya habari vya
kitaifa na kimataifa walivyomtafuta na
kumhoji.
Watanzania wametoa pongezi nyingi
kwa Getrude na kusema ni hazina ya
nchi, hadi sasa kwani amesaidia
kuitangaza nchi duniani kutokana na
hotuba hiyo aliyotoa mbele ya Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ki-moon.
Akizungumzia safari yao, Katibu Mkuu
wa Shirika la Mtandao wa Watoto na
Vijana Mwanza, Brightius Titus
anasema walimuandaa vizuri mtoto
huyo kwa kufanya mazoezi katika
ukumbi huo siku moja kabla ya
mkutano.
Anasema mara baada ya kutoa hotuba
hiyo watu kadhaa walimfuata
kumpongeza akiwa njiani kuelekea
hotelini na hata alipofika. Titus
anasema nia ya shirika hilo ni
kuendeleza jitihada za mtoto huyo kwa
kumpa nafasi ya kwenda mbele zaidi
na kuwa mfano kwa watoto na vijana
wa Kitanzania. Anamshukuru Balozi wa
Tanzania nchini Marekani kwa kumuita
nyumbani kwake na kumpongeza
pamoja na ofisi ya Makamu wa Rais
iliyomuita katika ofisi hizo mara tu
baada ya kuwasili nchini.
Baada ya kuwasili serikali ilitoa pongezi kwa kumuarika kushuhudia kikao kimoja cha byngr na pia mmoja ya waziri wa jamhuri ya muungani wa Tanzania ameahidi kumsomesha binti huyu.

1 Mei 2016

MFAHAMU 'MOHAMMED IQBAL' MTU ALIEBUNI NENO 'TANZANIA' MPAKA KUTUMIKA KAMA JINA LA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR.

Huyu bwana aliyebuni jina la Tanzania ni
Muhindi na dini yake ni AHMADIYA MUSLIM. Majina yake
ni MOHAMMED IQBAL DAR.
Mohammed alizaliwa Mkoani Tanga miaka
ya 1944,Baba mzazi wa Mohammed
alikuwa Daktari huko mkoani Morogoro
alikuwa anaitwa Dr. T A DAR alikuwa
Tanganyika kuanzia mwaka 1930.
Mohammed Iqbal Dar alipata elimu yake
ya Msingi Mkoani Morogoro shule ya
Msingi H H D AGAKAN kwa sasa ni Shule
ya Serikali na baada ya Hapo alikuja
baadae kujiunga na Chuo cha Mzumbe
akasoma Kidato cha Kwanza mpaka cha
Sita.
Aliingiaje kwenye shindano la
kupendekeza jina la Muungano kati
Tanganyika na Zanzibar,Mohammed
anasema alikuwa Maktaba akijisoma
gazeti la Tanganyika Standard siku hizi
Daily News akaona Tangazo linasema
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
unafahamika kama Republic of
Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana
refu sana kwa hiyo Wananchi wote
wakaombwa Washiriki kwenye shindano la
Kupendekeza jina moja litakalo zitaja nchi
zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar
Mohammed Iqbal Dar anasema aliamua
kuingia kwenye Shindano na hivi ndivyo
alianza Safari ya Kubuni Jina la
Muungano,Kwanza anasema alichukua
karatasi akaandika Bismillah Raahman
Rahimu hii ni kutokana na Imani yake na
baada ya hapo akaandika jina la
Tanganyika baada ya hapo akaandika
Zanzibar halafu akaandika jina lake Iqbal
halafu akaandika jina la Jumuiya yake ya
Ahmadiya baada ya Hapo akamrudia tena
Mwenyezi Mungu akamwomba amsaidie ili
apate jina zuri kutoka katika majina hayo
aliyokuwa ameyaandika.
Baada ya hapo Mohammed Iqbal Dar
alichukua herufi tatu kutoka Tanganyika
yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar
akachukua Herufi tatu za Mwanzo ZAN
ukiunganisha unapata TANZAN alivyoona
hivyo akachukua I herufi ya kwanza katika
jina lake la Iqbal na akachukua A kutoka
jina la dini yake yaani Ahmadiyya kwa
maana hiyo ukiongeza herufi hizi mbili I na
A kwenye TANZAN unapata jina kamili
TANZANIA akalisoma jina akaliona ni zuri
lakini akajiridhisha pia kwamba akiongeza
herufi hizo za I na A kwenye TANZAN
italeta maana kwakuwa nchi nyingi za
Afrika zinaishia na IA.
mfano
EthiopIA, ZambIA,NigerIA,TunisIA,SomalIA,GambIA,NamibIA,LiberIA,MauritanIA
alivyoona hivyo akaamua apendekeze
kuwa jina TANZANIA ndio litumike
kuwakilisha nnchi hizi mbili yaani
Tanganyika na Zanzibar kwa maana hiyo
jina TANZANIA limezaliwa kutoka majina
manne majina hayo ni
Tanganyika,Zanzibar,Iqbal na Ahmadiyya
Mohammed Iqbal Dar baada ya kupata
jina hilo akalituma jina hilo kwenye kamati
ya kuratibu Shindano
Baada ya Muda mwingi kupita baba yake
na Mohammed Iqbal Dar alipokea Barua
nzito kutoka serikalini ikiwa inasomeka
kama ifuatavyo….
REPRESENTED BY THE
MINISTRY OF
INFORMATION AND TOURISM,TANZANIA
TO
MOHAMED
IQBAL DAR
IN RECOGNATION OF THE
ACHIEVEMENT OF CHOOSING THE NEW
NAME FOR THE
UNITED REPUBLIC
OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR NAMELY
“REPUBLIC
OF TANZANIA”
DURING THE NATIONAL
COMPETITION DAY IN 19 TH NOVEMBER
1964
I A
WAKAL
MINISTER FOR
INFORMATION AND TOURRISM
Barua hiyo pia ilisema..
Utakumbuka kuwa miezi michache iliyopita
ulituandikia kutupa ushauri kuhusu jina
jipya la Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar na wewe pamoja na wananchi
wenzio 16 ulishauri nnchi yetu iitwe
Tanzania.Nafurahi kukuarifu kuwa
mshirikiane ile Zawadi y ash.200
iliyoahidiwa na leo nakuletea check ya
sh.12/50 ikiwa ni hisa yako katika zile
sh.200.Nashukuru sana kwa jitihada ya
kufikiri jina la Jamuhuri yetu
Barua ikasainiwa na Idrisa Abdul Wakil
Waziri wa Habari na utalii kipindi hicho.
Sasa kwa nini Mohamedi Iqbal Dar anadai
yeye kuwa mshindi pekee wakati Barua
ilikuwa inaonyeshakulikuwa na washindi
wengine 15 ambao nao walishinda,Jibu ni
kuwa wakati wa kutolewa kwa Zawadi hizo
hakuna aliyejitokeza zaidi ya Bwana
Mohammed Iqbal Dar na Bwana Yusufal
Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa
sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya
kumpongeza kuwa ameshinda kwa madai
kuwa Barua ameipoteza,hivyo Wizara ya
Habari na Utalii iliamua kumtangaza
bwana Mohammed Iqbal Dar kuwa Mshindi
na kumpatia zawadi yote y
ash.200/:pamoja na Ngao.
Bwana Mohammedi Iqbal Dar anasema
anachosikitika ni kuwa Mchango wake
bado Watanzania hawathamini mchango
wake lakini yeye anaipenda Tanzania na
anajivunia kuwa Mtanzania japo anadhani
dini yake ya Uislamu ndio tatizo hawataki
kutambua mchango wake ila anaamini
kuwa siku moja ukweli utajulikana
Hayo ni maelezo ya Mohammed Iqbal Dar
ambaye kwa sasa anaishi Uingereza kwa
kuwa huko ndiko alipata kazi eneo la
Birmigham b35 6ps UK,Dar –es-Salaam
House,18 TURNHOUSE ROAD,PHONE 44
121-747-9822.